Jumamosi, 14 Februari 2015


Kikao cha CCM kilichowahusisha Vijana,Waujumbe wa CCM Kata na viongozi wengine wa CCM Wilayani 12/0215 akiwemo Mheshimiwa Waziri na Mbunge wa Jimbo la Kyela Dkt Harrison G.Mwakyembe na Mwenyekiti wa Chama Wilaya mheshimiwa Hunter Mwakifuna. Tumefanikiwa kupata kile kilichozungumzwa ndani ya kikao hicho na wazungumzaji wawili. 1.Mwenyekiti wa CCM wa CCM wilaya ndugu Hunter Mwakifuna
Kikao kilifunguliwa na Mwenyekiti wa CCM Wilayani. Mwenyekiti alitumia muda mwingi kwa kumpamba Mh. Mwakyembe na kusema kwamba CCM Kyela tayari ina Mtambua Mwakyembe kama Mgombea wao 2015,hakuna aja ya kubadilisha wakati anafanya vizuri kwani hii ni nguo? Aliuliza Mwenyekiti.Nimetembea nchi nzima kila mtu anasema Kyela tuna bahati sana kwa kupata Mbunge kama Mwakyembe,Maendeleo aliyoyaleta Mbunge wetu hakuna mbunge mwingine Tanzania,aliendelea kutamba huyo Mwenyekiti.
2.Mbunge waJimbo la Kyela Mh. Dr.Harrison Mwakyembe Mh,Alianza kwa kujigamba mbele ya Wajumbe na kama kawaida yake akanza na ahadi kibao na mambo waliyoyafanya mpaka sasa hivi -Kuna nafasi za kazi 200 zinasubiri vijana wa Kyela
-Mgodi wa makaa ya mawe utafunguliwa mwaka huu na kazi zote watapewa wana Kyela.
-Kila kata tutatoa pikipiki ili kuendeleza chama na kusaidia wakati wa kampeni
-Kila kijiji baiskeli
-Tumetengeneza barabara nzuri na za kudumu na tunaendelea kujenga kwa viwango bora.
-Watu wanasema daraja walijenga wanajeshi wakati mi ndo niliongea na mkuu wa majeshi ili wanajeshi wasaidie.
-Watu wengi Tanzania wananiomba mimi nigombee urais maana wajua kwamba mimi ni mchapa kazi na ninauwezo na kama ikitokea kwamba sitagombea ubunge kyela,nitaakikisha nawaletea mtu wa maana na mchapa kazi kama mimi.
-Kuna upoteshaji mwingi kuhusu mabadiliko ya wizara.Nikwamba kuna matatizo mengi ndani ya huu umoja wetu wa Afrika Mashariki.sasa rais akaona amtume mtu makini na mwenye uwezo na uzoefu si mnajua nilikuwa uko kabla ya kugombea hapa. Mwisho sisi wanyakyusa tukikutana tunapeana maji ya kunywa kama hakuna chakula,kwahiyo kila mjumbe atapata elfu kumi za maji.Asanteni Mwenyekiti alisimama na kufunga kikao kwa kusema HAKUNA MASWALI KIKAO KIMEFUNGWA. Source Mjumbe wa CCM Kata aliyekuwemo ndani ya Kikao

Ijumaa, 30 Januari 2015


Mkuu wa Wilaya ya Kyela Bi Simalenga katikati mwenye suti Nyekundu,kushoto ni mwakilishi wa Mwenyekiti Kamati ya shule na Nyuma kabisa ni Mkuu wa Shule Bwana N.Sedekia pamoja na Wanafunzi na Wageni Wengine katika picha ya pamoja kwenye Tranfoma walipochukulia Umeme kuupeleka Shuleni mita chache kutoka hapo

Mkuu wa Wilaya akizindua kwa kuwasha Swichi kuu(Main Switch) Shuleni Mwaya

Mkuu wa Wilaya , Mwenyekiti wa Kamati ya shule, mkuu wa Wilaya na Kiongozi wa Skauti shuleni wakielekea kwenye Tranfoma palipochukuliwa Umeme
Mkuu wa wilaya ya Kyela Bi Magreth Simalenga leo asubuhi amezindua Nishati ya umeme katika Shule ya Sekondari Mwaya iliyopo Tarafa ya Ntebela Wilayani Kyela.Nishati ya Umeme katika Shule hiyo imekuwa ni moja ya changamoto ya muda mrefu kwa Waalimu na Wanafunzi hasa kwa kuzingatia kuwa shule hii imekuwa ikipata msaada kutoka kwa wadau mbalimbali. Miaka michache iliyopita Shule ya sekondari Mwaya ilipata msaada wa Kompyuta Mpakato kutoka shirika la Kimataifa lililoko nchini Marekani liitwalo Chocolate.
Hata hivyo licha ya msaada huo na mingine mingine mingi shule hiyo imekuwa ikikutana na Changamoto kubwa ya nishati hasa ya Umeme kwa ajili ya kusaidia uendeshaji na uendelezaji wa misaada hiyo ili kuleta tija kwa Wanafunzi hao. Umeme huo uliochukuliwa kutoka mita chache shuleni umezinduliwa na Mkuu wa Wilaya ya Kyela na kushuhudiwa na wanafunzi na Mkuu wa Shule Bwana.N.Sedekia na Mwenyekiti wa Kamati ya shule.
Kupatikana kwa Umeme huo kunatarajiwa kuchangia kuongezeka kwa kiwango cha ubora wa Elimu itolewayo shuleni hapo na pia kupunguza Uzembe wa wanafunzi kwa maendeleo yao Binafsi.

Jumamosi, 10 Januari 2015

Hali ya Sintofahamau ilitokea wilayani Kyela siku a January 8 mida ya saa tisa alasiri katika mamlaka ya mji mdog na maeneo ya ofisi za CCM wilayani Kyela ambapo Askari wa kutuliza ghasia(FFU)kutoka jijini Mbeya ilibidi waingie kazini. Hayo yalifanyika mbele ya Mbunge na Waziri wa Uchukuzi Dr.Harison Mwakyembe
Mtandao wako wa Nyumbani ukiongea na baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wametuhabarisha kuwa Vurugu hizo zimesababishwa na Kitendo cha Chama chA Mapinduzi kutaka kuongeza wajumbe wanne katika uchaguzi wa Baraza la Mji mdogo waKyela ambao ni pamoja na mbunge wa jimbo hilo Dr.Harison Mwakyembe na madiwani wa CCM watatu hivyo kuwa na wajumbe wa ziada wanne . Mashuhuda wamezidi kudpokeza kuwa sababu kubwa za Vurugu na Tfrani hizo zilizopelekea Mheshimiwa mbunge kutupiwa mawe ni;
Kwanza, Kisheria wajumbe hao wanaruhusiwa kuwa wajumbe wa Baraza la Mamlaka ya mji mdogo lakini hawatakiwa kushiriki katika kuunda Baraza hilo maana bado halijaundwa .
Pili, Kwanini upande wa Madiwani watatu wote watoke Chama Cha Mapinduzi?
Hata hivyo uchaguzi huo uliahirishwa ili wataalamu wa Sheria wakatafsiri upya Sheria na kuwezesha Barza la mji mdogo kuundwa. Katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa ndani ya mamlaka hiyo Chama cha Demikrasia na M,aendeleo kimetwaa viti 29 na Cham cha Mapinduzi kimetwaa viti 26 hivyo kuonesha waziwazi kuwa CHADEMA Inaweza kushinda na kuliongoza Baraza la Mamlaka ya mji mdogo Kyela.
Wakati huohuo MWAKYEMBE AWAONYA CHADEMA
Jana akizungumza na clouds FM amewataka Chadema kuacha ujinga wa kuchukua watu toka mkoa wa kilimanjaro na kwenda kupiga kambi Kyela.
Mh Mwakyembe amesema CHADEMA Kyela iache kuwatumia vijana toka Moshi waliopiga kambi Kyela!! Ameyasema haya wakati akihojiwa na Clouds kwenye Power Breakfast!!
Amesema ni ujinga kwa chama kikuu cha upinzani kuendelea kutumia wakazi wa mkoa wa kilimanjaro kukinadi chama kwani hawajui tamaduni za makabila mengine hivyo ipo siku wataumbuka.
Amedai kama si huruma yake wachaga hawa toka machame walioenda Kyela kumchafua angeweza kuwapoteza kabisa na amewakanya kutokufika tena jimboni huko kwa shughuli za kisiasa kwani licha ya kuwa anapendwa na wanakyela wenyewe pia Tanzania nzima inaona kazi anayoifanya hivyo si rahisi kulipta jimbo hilo kama wanavyodhani.
Amewataka kutafuta watu wasomi wanaojua statistics/Takwimu ili wawaelekeze mahali pa kwenda kwa kutumia Takwimu si wanakurupuka tu