
JESHI la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limeleezea namna mwanajeshi wake, Meja Khatibu Shaaban Mshindo, alivyouawa baada ya kuangukiwa na bomu, wakati akiwa katika jukumu la ulinzi wa amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Pamoja
 na hayo, Watanzania wametakiwa kuimarisha mshikamano na kuachana na 
makundi yenye nia ya kuleta mgawanyiko, hasa katika kipindi hiki kigumu 
ambacho Tanzania imepoteza askari wake waliopewa dhamana ya kitaifa ya 
ulinzi wa amani katika nchi zenye migogoro Afrika.
Akitoa
 salamu za rambirambi wakati askari huyo wa kikosi cha Mizinga namba 83 
KJ kilichopo Kibaha akiagwa rasmi kijeshi Dar es Salaam jana, Mkuu wa 
Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamnyange, alisema askari huyo pamoja
 na askari watano wa Tanzania, waliangukiwa na bomu hilo na kujeruhiwa 
vibaya.
“Waliangukiwa
 na bomu Agosti 28, mwaka huu huko Goma DRC eneo walilokuwa wakifanyia 
kazi… Meja Mshindo aliumia vibaya na kukutwa na mauti njiani akipelekwa 
hospitalini,” alisema Jenerali Mwamunyange.
Alisema
 katika tukio hilo, askari wengine watano wa Tanzania walijeruhiwa 
vibaya na wanaendelea vizuri na matibabu nchini humo na hali zao 
zinaendelea vizuri.
Akimzungumzia
 Meja Mshindo, Jenerali Mwamunyange alisema katika uhai wake alikuwa 
mchapakazi, muaminifu, hodari na mtiifu na kifo chake kimetokea wakati 
jeshi linamhitaji.
“Kifo
 chake kimeacha pengo ndani ya JWTZ na itachukua muda mrefu kuziba pengo
 hili.” Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard 
Membe, alisema kifo cha askari huyo ni msiba wa kitaifa na kumtaja Meja 
Mshindo kuwa shujaa aliyekutwa na mauti wakati akitekeleza kazi 
aliyotumwa na nchi yake.
Alisema
 kifo hicho pamoja na vifo vya askari wengine saba wa JWTZ vilivyotokea 
Darfur mwaka huu, ni chachu kwa Tanzania kuendeleza jitihada za kusaidia
 nchi zenye migogoro na kuhamasisha amani Afrika.
“Serikali inapata matumaini namna Watanzania walivyosimama pamoja na kuunga mkono jeshi letu katika kipindi hiki kigumu. Ingekuwa nchi nyingine, haya yaliyotokea yangeleta mgawanyiko mkubwa miongoni mwa raia, lakini kwa hapa kwetu hali imekuwa tofauti,” alisema Membe.
Aliwataka
 wachache wenye mawazo ya kutumia matukio hayo kuwagawa Watanzania, 
waache mara moja nia yao hiyo, kwa kuwa moja ya kazi ambayo Tanzania 
inayo, ni pamoja na nia yake ya kuhamasisha na kutangaza amani Afrika na
 dunia kwa ujumla.
“Jamani
 wajibu wetu ni kuhakikisha haya maeneo yenye migogoro yanakuwa na 
amani, kule DRC hali ni mbaya, watu wanakufa kila kukicha na akinamama 
na watoto wanabakwa na kudhalilishwa, sasa sisi kama taifa ni vyema 
kujitokeza na kusaidia wenzetu,” alisisitiza.
Meja
 mshindo, alizikwa jana nyumbani kwao Fujoni Zanzibar na ameacha mke 
mmoja, Hawa Mnimbo na watoto watatu ambao ni Shaaban, Abuu na Samir 
Mshindo
Jumanne, Septemba 03, 2013
Unknown
0 comments :
Chapisha Maoni