Mtanzania Agnes Gerald, maarufu Masogange, ameachiwa huru na Mahakama ya Kempton ya jijini Johannesburg, baada ya kulipa faini ya R30,000 (Sh4.8 milioni) kwa kosa la kubeba kemikali zinazotumika kutengeneza dawa za kulevya.
Wakati Masogange akitozwa faini hiyo mwenzake, 
Melissa Edward ameachiwa huru na mahakama hiyo, baada ya kukosekana 
ushahidi wa kumtia hatiani.
                
              
Msemaji wa Kitengo cha Uchunguzi wa Makosa ya 
Jinai cha Afrika Kusini(Hawk), Kapteni Paul Ramaloko alisema Watanzania 
hao wameachiwa huru baada ya kuonekana kuwa hawakubeba dawa za kulevya, 
bali kemikali aina ya ephedrine.
                
              
Hata hivyo, Mahakama ilibaini kuwa, Melissa hana 
hatia kwa kuwa ilionekana kuwa amemsindikiza Masogange, ambaye alimwomba
 amsaidie kubeba mzigo huo.
                
              
“Mahakama iliona kuwa Melissa aliombwa tu 
kumsaidia kubeba baadhi ya mabegi, lakini hayakuwa yake. Mizigo yote 
iliandikwa jina la Agness Gerald na si Melissa,” alisema Kapteni 
Ramaloko.
                
              
Kapteni Ramaloko alisema, Melissa alijitetea kuwa 
hakuwa amesafiri pamoja na Masogange bali walikutana ndani ya ndege na 
Masogange alimwomba amsaidie kubeba mizigo hiyo, kwani ilikuwa mikubwa.
                
              
Kwa sheria za Afrika Kusini kubeba kemikali zozote
 ambazo zimepigwa marufuku ni kosa la jinai kisheria, hivyo mahakama 
iliamuru Masogange ahukumiwe kwenda jela kwa miezi 30 (miaka miwili na 
miezi mitano) au alipe faini ya R30, 000 (sawa na Sh4.8 milioni).
                
              
Hata hivyo, Kapteni Ramaloko alisema mdhamini wa Masogange alilipa nusu ya fedha na kwamba zinazobaki amalizie baadaye.
                
              
Alisema kutokana na kutomalizia kulipa fedha hizo 
ataendelea kubaki nchini humo hadi atakapomaliza kulipa nusu ya faini 
iliyobaki.
                
              
Masogange na mwenzake walipokamatwa na SARS ilielezwa walikuwa wamebeba dawa za kulevya aina ya
                
              
Methamphetamine, lakini Mahakama juzi ilithibitisha walikamatwa na kemikali aina ya Ephedrine, ambayo siyo dawa za kulevya.
                
              
Wakati Kamishna Mkuu wa Kitengo cha Kudhibiti Dawa
 za Kulevya nchini, Geofrey Nzowa alipoulizwa na Mwananchi Jumamosi juzi
 alisema mzigo walioubeba Masogange na mwenzake haukuwa ni dawa za 
kulevya bali ni kemikali za dawa za kulevya, lakini Msemaji wa Mamlaka 
ya Mapato ya Afrika Kusini, (SARS), Marika Muller alieleza kuwa timu ya 
SARS ina uhakika kuwa mabegi sita yaliyokamatwa Julai 5 ni dawa za 
kulevya aina ya Methamphetamine.
Jumamosi, Septemba 21, 2013
Unknown

0 comments :
Chapisha Maoni